TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
TAMKO rasmi la Ndugu Zitto Z. KABWE (MB) kuhusiana na kinachoitwa "Taarifa ya Siri ya Chadema"
Ndugu Wanahabari,
NILIPOKUWA katika ziara ya bara la Ulaya kati ya Oktoba 21 mpaka Novemba 2 mwaka huu (2013), nilipokea kwa njia ya barua pepe ripoti inayoitwa "Taarifa ya Siri ya Chadema" ambayo pia ilikuwa imesambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii.
“Taarifa ya Chadema inasema kwamba chama hicho (chama changu) kilikuwa kimechunguza mwenendo wangu tangu mwaka 2008 hadi 2010 na kubaini kuwa mimi napokea fedha kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kuivuruga Chadema.
Ripoti hiyo ilinihusisha pia na mwananchi raia wa Ujerumani, Andrea Cordes ambaye, kwa mujibu wa ripoti hiyo, alinisaidia kupokea na kuhifadhi kiasi cha dola 250,000 za Marekani kupitia kwenye akaunti yake binafsi.
Taarifa hii ya kutunga na iliyojaa uongo wa kiwango cha kutisha, imenifadhaisha, kunisikitisha na kunikasirisha.
Taarifa hii iliibuliwa katika kipindi ambacho nilikuwa safarini kutetea haki za Watanzania na Waafrika ambao utajiri wao wa rasilimali unafaidiwa na watu wachache waliohifadhi mali katika nje za nje na pia kupigania makampuni ya mataifa tajiri yalipe kodi stahiki katika nchi zetu.
Pengine lengo la ripoti hiyo lilikuwa ni kutaka kunipoteza kutoka katika nia na dhamira yangu ya dhati ya kutaka Watanzania wafaidike na utajiri wao. Muda ambao watunzi wa ripoti hiyo waliamua kutoa taarifa yao unazua maswali mengi kuliko majibu.
Nafahamu kwamba mimi ni mwanasiasa ambaye nimekuwa mlengwa (target) wa mashambulizi kutoka kwa makundi mbalimbali ya wanasiasa na vikundi vyao. Kama mwanasiasa, niko tayari kupokea changamoto zozote zinazokuja na uanasiasa wangu.
Hata hivyo, ambacho sitakubali ni kwa watu kutumia jina langu na uanasiasa wangu kunichafua mimi binafsi na watu wengine wasiohusika kwa sababu ya kutaka kutimiza malengo yao ya kidhalimu.
Raia huyo wa Kijerumani tayari amekana kuhifadhi fedha zangu. Kwa maelezo yake kwa baadhi ya viongozi wa Chadema amekana kuwa na akaunti inayotajwa na amekana pia kuwepo nchini Ujerumani katika siku na wakati uliotajwa kwenye ripoti hiyo.
Ripoti hiyo imemtaja pia mtu kama Dk. Charles Kimei, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB ikidai kwamba nilikutana naye na alishiriki kwenye igizo hilo la kunipa fedha.
Niseme mapema kwamba tangu kuzaliwa kwangu sijawahi hata mara moja kukutana na Dk. Kimei popote pale ndani au nje ya nchi. Kumuingiza mtu ambaye amejenga jina lake kwenye taaluma ya kibenki kwa sababu tu ya lengo ovu la kumchafua Zitto Zuberi Kabwe si uungwana bali ni unyama.
Kutokana na uchafuzi huu wa wazi dhidi ya taswira yangu binafsi na watu wengine walioingizwa kwenye mkumbo huu, nimeandika rasmi kwa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk.Wilbrod Slaa kumwomba athibitishe kwamba kinachoitwa Taarifa ya Siri ya Chadema ni kweli ni taarifa ya chama au kiikanushe ili niweze kuchukua hatua za kisheria dhidi ya waandishi wa hekaya hiyo.
Cha ajabu, nimepokea ujumbe wa kutishiwa maisha kutoka kwa mtu anayejiita Theo Mutahaba na kuahidiwa KUPOTEZWA endapo nitaendelea na jitihada zangu za kupambana na ufisadi na kutafuta haki kwa Watanzania wote pasipo kujali tofauti zao za kiitikadi, kikanda, kikabila na kidini.
Natarajia kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya wote ambao wamehusika na utungaji na uenezi wa taarifa hii. Nitahakikisha kwamba wahusika wanatafutwa na kufunguliwa mashitaka stahiki ya upotoshaji na kuchafuana.
Ni matarajio yangu kwamba wale wenye mapenzi mema na Tanzania, mimi binafsi na utawala wa sheria, wataelewa nia yangu ya kutafuta haki katika suala hili.
Nimeamua kujitolea maisha yangu kwa ajili ya Watanzania na kama alivyopata kusema Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela; “Struggle Is My Life.”
Forward Ever, Backward Never- Kwame Nkrumah
Zitto Kabwe (Mb)
TAMKO
LA HAKIELIMU KUHUSU UPANGAJI WA VIWANGO VYA ALAMA, MATUMIZI YA ALAMA
ENDELEVU YA MWANAFUNZI NA UFAULU
4 NOVEMBA 2013.
Hivi karibuni serikali imetoa tamko kuhusu mfumo mpya wa upangaji wa
viwango vya alama, matumizi ya alama endelevu ya mwanafunzi na ufaulu.
HakiElimu na wadau wake imetafakari tamko hilo na kutoa maoni ya
yafuatayo:
1. Hatujatambua lengo la serikali kuleta mabadiliko
haya; hasa ikikumbukwa kuwa Tume ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mh. Mizengo
Pinda haijawahi kuweka bayana taarifa yake kuhusu sababu za wanafunzi
kutofaulu vizuri katika mitihani ya kumaliza kidato cha nne. Wajumbe wa
Tume hiyo wamekuwa wakitoa dondoo fupi fupi za matokeo ya kazi yao-kama
vile Bungeni na katika hadhira nyingine za kitaifa; bila kutoa ripoti
yenyewe. Je, kwa mabadiliko haya,wizara inataka kuwaaminisha Watanzania
kwamba alama zilivyokuwa zimepangiliwa hapo awali,ndiyo sababu kuu ya
wanafunzi kutofaulu vizuri?
2. Wizara imeeleza kwenye tamko
lake kwamba imeshirikisha wadau mbalimbali katika kufikia uamuzi huo.
Hata hivyo, katika orodha ya wadau walioshirikishwa inaonekana bayana
kuwa asasi za utetezi hazikupewa nafasi. Baada ya kufanya mawasiliano na
baadhi ya wadau wanaodaiwa kushiriki,wenyewe wamekiri kuwa ingawa
walishiriki mawazo yao hayakuzingatiwa na hawakukubaliana kuhusu
kushusha alama za ufaulu kufikia 20 kati ya 100.
3. Mpangilio
wa alama zitakazotumika kuanzia mwaka huu unaleta tafsiri ya ndani
kuhusu nia ya wizara kubadilisha alama hizo. Tafsiri hiyo ni kulazimisha
kuona kwamba wanafunzi wachache zaidi wanapata daraja la 5 (ambalo
limeanzishwa badala ya daraja sifuri); kukiwa na uwezekano wa kupunguza
wanafunzi wanaopata daraja hili kwa asilimia 2.2% ukilinganisha na
utaratibu uliotumika kwa matokeo ya mwaka 2012. Mpangilio huo mpya una
uwezekano wa kuongeza kundi la wanafunzi wanaopata daraja la tatu na la
nne kwa asilimia 12.1% kuliko utaratibu uliotumika mwaka 2012. Hata
hivyo, alama hizo mpya zinaweza kupunguza uwezekano wa kupata daraja la
kwanza na la pili kwa asilimia 11.9%. Serikali na wadau wengine wa elimu
wanatambua bayana kuwa njia kuu ya kuboresha elimu na matokeo katika
mitihani ni kuboresha utaratibu wa utoaji wa elimu. Kwa nini serikali,
hasa katika kipindi hiki inataka kuona matokeo mazuri bila kuwekeza
kwenye mipango ya kuboresha mfumo na utaratibu wa utoaji wa elimu?
HakiElimu inatafsiri uamuzi huo wa serikali kama ni kukwepa ukweli na
utaalamu; na badala yake serikali inatafuta njia ya mkato ya
kuwafurahisha wazazi na wananchi ili wapunguze kelele.
4.
Serikali imekubali kutumia asilimia 40 kutoka kwenye Alama za Tathmini
Endelevu ya Mwanafunzi (Continuous Assessment, CA), ili ziunganishwe na
alama 60 za mtihani wa mwisho. Hata hivyo, uzoefu unaonesha kuwa alama
hizo zilikuwa zinachakachuliwa huko shuleni, na hata Baraza la Mitihani
Tanzania mwaka huu walikiri hilo kutokea. Wizara ya Elimu na Mafunzo ya
Ufundi itatumia njia gani kuhakikisha kuwa zinapatikana alama sahihi
toka shuleni zinazoendana na uwezo wa mwanafunzi? Je, kwa kiasi gani
walimu wameandaliwa na kujengewa mazingira mazuri ya kufanikisha zoezi
hili? Hata hivyo, serikali inapaswa pia kuwaeleza watanzania uzoefu wa
nchi nyingine za Afrika katika matumizi ya alama za CA; wengine
wanatumia asilimia ngapi? Ni muhimu kuwa na ushahidi kuwa kiwango cha CA
tutakachokitumia kitaboresha utaratibu wa kutathmini wanafunzi; na
kuwatendea haki badala ya kuwaghiribu au kuwaumiza.
5.
HakiElimu inasikitika kuona wizara inalazimisha kila mwanafunzi
atakayefanya mtihani wa kidato cha nne au cha sita awe amefaulu. Hiyo
inathibitishwa na tafsiri ya alama ambazo zitatumika zinazoonesha kwamba
kuanzia atakayepata alama sifuri mpaka mia moja atakuwa amefaulu kwa
namna fulani. Kwa mfano, hata atakayepata alama kuanzia 0 mpaka 19
katika somo fulani atahesabiwa kuwa amefaulu, japo katika kiwango
kisichoridhisha. Kwa nini wizara inakosa ujasiri wa kukubali kuwa
mwanafunzi atakayepata chini ya alama fulani ahesabiwe kuwa hakufaulu?
6. Kwa upangaji huo mpya wa alama za ufaulu, Tanzania itakuwa nchi ya
kwanza katika bara la Afrika kwa kuwa na kiwango cha chini kabisa cha
ufaulu katika elimu ya sekondari na kuna hatari kwamba kushushwa kwa
alama za ufaulu kutapunguza ama kuondoa hamasa ya wanafunzi kusoma kwa
bidii, kwa kuamini kuwa hawatafeli na cheti watapata tu. Kama wadau wote
tunakubaliana kuwa nia ya kutoa elimu ni kuandaa Watanzania ambao
watakuwa na maarifa na uwezo wa kushindana na wengine wanaosoma katika
nchi nyingine Afrika.
7. HakiElimu pia inasikitika kuona kuwa
wizara inapotosha malengo ya “Matokeo Makubwa Sasa (Big Results
Now-BRN)” kwa kutafuta njia za mkato. BRN imeeleza bayana kuwa kati ya
mikakati itakayotumika kupata Matokeo Makubwa katika elimu ni kuboresha
mchakato wa kufundisha na kujifunza shuleni na kuboresha utaratibu wa
utoaji wa elimu kwa kuweka bayana majukumu ya Wizara ya Elimu na Mafunzo
ya Ufundi na ile ya TAMISEMI. Wizara iwaambie Watanzania kuwa kwa kiasi
gani upangaji huu wa alama utasaidia kuboresha mazingira ya ufundishaji
na ujifunzaji kwa maana ya kumjengengea mwalimu uwezo, mazingira mazuri
na hamasa ya kufundisha na pia kutengeneza mazingira mazuri ya
mwanafunzi kujifunza. Katika haya, je, ni kweli kwamba huu upangaji upya
wa madaraja ni kipaumbele chetu namba moja? Si busara kushughulikia
mpangilio wa alama na madaraja kwanza wakati mchakato wa kuboresha mfumo
wa elimu ili kupata hayo matokeo mazuri bado uko chini. Kitendo hicho
ni kukurupuka na kuruka hatua muhimu zinazoweza kuboresha elimu.
8. HakiElimu inawatahadharisha Watanzania, wakiwemo wazazi, wanafunzi
na vijana wenye nia ya kurudia mitihani ili wapate vyeti; na serikali
yenyewe kuzingatia ukweli kwamba: Elimu ni uwezo, SIYO cheti. Jitihada
za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi zinaonesha wazi kuwa nia ni
kuona matokeo mazuri hata kama matokeo hayo hayataendana na uwezo walio
nao wanafunzi. Katika kutengeneza raslimali watu ya kutosha, Tanzania
kama ilivyo kwa nchi nyingine haina namna ya kukwepa kuhakikisha kwamba
mfumo wa elimu unaandaa vijana au wananchi wenye uwezo wa kukabiliana na
changamoto zinazowakabili wao wenyewe, jamii na Taifa kwa ujumla; pia
kuwa na wananchi ambao watakuwa na ujasiri, tija na ubunifu, katika
uzalishaji katika shughuli na fursa mbalimbali watakazozipata au
kuzitafuta. Hali hii haipatikani kwa kuhangaika na alama za ufaulu kama
kipaumbele. Tunahitaji kuhangaika na mfumo wa utoaji elimu
utakaotusaidia kuleta mapinduzi ya kweli ya kiuchumi, kijamii na
kisiasa.
HakiElimu inaishauri Serikali kusitisha matumizi ya
alama na madaraja haya mapya. Irudi kwa wadau na ushahidi kuhusu uamuzi
huu; huku ikitoa nafasi ya kuchukua maoni ambayo yanaweza kuboresha
mfumo wa upimaji wa wanafunzi. Wakati zoezi hilo linaendelea, HakiElimu
inaisisitiza Serikali kutumia matokeo ya tafiti mbalimbali na mipango
iliyopo kushughulikia dosari na changamoto zinazorudisha nyuma elimu
yetu, hasa zile zinazokwamisha ufundishaji na ujifunzaji shuleni.
Tamko hili limesainiwa na,
Elizabeth Missokia Mkurugenzi Mtendaji, HakiElimu
4 NOVEMBA 2013.
Hivi karibuni serikali imetoa tamko kuhusu mfumo mpya wa upangaji wa viwango vya alama, matumizi ya alama endelevu ya mwanafunzi na ufaulu. HakiElimu na wadau wake imetafakari tamko hilo na kutoa maoni ya yafuatayo:
1. Hatujatambua lengo la serikali kuleta mabadiliko haya; hasa ikikumbukwa kuwa Tume ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mh. Mizengo Pinda haijawahi kuweka bayana taarifa yake kuhusu sababu za wanafunzi kutofaulu vizuri katika mitihani ya kumaliza kidato cha nne. Wajumbe wa Tume hiyo wamekuwa wakitoa dondoo fupi fupi za matokeo ya kazi yao-kama vile Bungeni na katika hadhira nyingine za kitaifa; bila kutoa ripoti yenyewe. Je, kwa mabadiliko haya,wizara inataka kuwaaminisha Watanzania kwamba alama zilivyokuwa zimepangiliwa hapo awali,ndiyo sababu kuu ya wanafunzi kutofaulu vizuri?
2. Wizara imeeleza kwenye tamko lake kwamba imeshirikisha wadau mbalimbali katika kufikia uamuzi huo. Hata hivyo, katika orodha ya wadau walioshirikishwa inaonekana bayana kuwa asasi za utetezi hazikupewa nafasi. Baada ya kufanya mawasiliano na baadhi ya wadau wanaodaiwa kushiriki,wenyewe wamekiri kuwa ingawa walishiriki mawazo yao hayakuzingatiwa na hawakukubaliana kuhusu kushusha alama za ufaulu kufikia 20 kati ya 100.
3. Mpangilio wa alama zitakazotumika kuanzia mwaka huu unaleta tafsiri ya ndani kuhusu nia ya wizara kubadilisha alama hizo. Tafsiri hiyo ni kulazimisha kuona kwamba wanafunzi wachache zaidi wanapata daraja la 5 (ambalo limeanzishwa badala ya daraja sifuri); kukiwa na uwezekano wa kupunguza wanafunzi wanaopata daraja hili kwa asilimia 2.2% ukilinganisha na utaratibu uliotumika kwa matokeo ya mwaka 2012. Mpangilio huo mpya una uwezekano wa kuongeza kundi la wanafunzi wanaopata daraja la tatu na la nne kwa asilimia 12.1% kuliko utaratibu uliotumika mwaka 2012. Hata hivyo, alama hizo mpya zinaweza kupunguza uwezekano wa kupata daraja la kwanza na la pili kwa asilimia 11.9%. Serikali na wadau wengine wa elimu wanatambua bayana kuwa njia kuu ya kuboresha elimu na matokeo katika mitihani ni kuboresha utaratibu wa utoaji wa elimu. Kwa nini serikali, hasa katika kipindi hiki inataka kuona matokeo mazuri bila kuwekeza kwenye mipango ya kuboresha mfumo na utaratibu wa utoaji wa elimu? HakiElimu inatafsiri uamuzi huo wa serikali kama ni kukwepa ukweli na utaalamu; na badala yake serikali inatafuta njia ya mkato ya kuwafurahisha wazazi na wananchi ili wapunguze kelele.
4. Serikali imekubali kutumia asilimia 40 kutoka kwenye Alama za Tathmini Endelevu ya Mwanafunzi (Continuous Assessment, CA), ili ziunganishwe na alama 60 za mtihani wa mwisho. Hata hivyo, uzoefu unaonesha kuwa alama hizo zilikuwa zinachakachuliwa huko shuleni, na hata Baraza la Mitihani Tanzania mwaka huu walikiri hilo kutokea. Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi itatumia njia gani kuhakikisha kuwa zinapatikana alama sahihi toka shuleni zinazoendana na uwezo wa mwanafunzi? Je, kwa kiasi gani walimu wameandaliwa na kujengewa mazingira mazuri ya kufanikisha zoezi hili? Hata hivyo, serikali inapaswa pia kuwaeleza watanzania uzoefu wa nchi nyingine za Afrika katika matumizi ya alama za CA; wengine wanatumia asilimia ngapi? Ni muhimu kuwa na ushahidi kuwa kiwango cha CA tutakachokitumia kitaboresha utaratibu wa kutathmini wanafunzi; na kuwatendea haki badala ya kuwaghiribu au kuwaumiza.
5. HakiElimu inasikitika kuona wizara inalazimisha kila mwanafunzi atakayefanya mtihani wa kidato cha nne au cha sita awe amefaulu. Hiyo inathibitishwa na tafsiri ya alama ambazo zitatumika zinazoonesha kwamba kuanzia atakayepata alama sifuri mpaka mia moja atakuwa amefaulu kwa namna fulani. Kwa mfano, hata atakayepata alama kuanzia 0 mpaka 19 katika somo fulani atahesabiwa kuwa amefaulu, japo katika kiwango kisichoridhisha. Kwa nini wizara inakosa ujasiri wa kukubali kuwa mwanafunzi atakayepata chini ya alama fulani ahesabiwe kuwa hakufaulu?
6. Kwa upangaji huo mpya wa alama za ufaulu, Tanzania itakuwa nchi ya kwanza katika bara la Afrika kwa kuwa na kiwango cha chini kabisa cha ufaulu katika elimu ya sekondari na kuna hatari kwamba kushushwa kwa alama za ufaulu kutapunguza ama kuondoa hamasa ya wanafunzi kusoma kwa bidii, kwa kuamini kuwa hawatafeli na cheti watapata tu. Kama wadau wote tunakubaliana kuwa nia ya kutoa elimu ni kuandaa Watanzania ambao watakuwa na maarifa na uwezo wa kushindana na wengine wanaosoma katika nchi nyingine Afrika.
7. HakiElimu pia inasikitika kuona kuwa wizara inapotosha malengo ya “Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now-BRN)” kwa kutafuta njia za mkato. BRN imeeleza bayana kuwa kati ya mikakati itakayotumika kupata Matokeo Makubwa katika elimu ni kuboresha mchakato wa kufundisha na kujifunza shuleni na kuboresha utaratibu wa utoaji wa elimu kwa kuweka bayana majukumu ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na ile ya TAMISEMI. Wizara iwaambie Watanzania kuwa kwa kiasi gani upangaji huu wa alama utasaidia kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji kwa maana ya kumjengengea mwalimu uwezo, mazingira mazuri na hamasa ya kufundisha na pia kutengeneza mazingira mazuri ya mwanafunzi kujifunza. Katika haya, je, ni kweli kwamba huu upangaji upya wa madaraja ni kipaumbele chetu namba moja? Si busara kushughulikia mpangilio wa alama na madaraja kwanza wakati mchakato wa kuboresha mfumo wa elimu ili kupata hayo matokeo mazuri bado uko chini. Kitendo hicho ni kukurupuka na kuruka hatua muhimu zinazoweza kuboresha elimu.
8. HakiElimu inawatahadharisha Watanzania, wakiwemo wazazi, wanafunzi na vijana wenye nia ya kurudia mitihani ili wapate vyeti; na serikali yenyewe kuzingatia ukweli kwamba: Elimu ni uwezo, SIYO cheti. Jitihada za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi zinaonesha wazi kuwa nia ni kuona matokeo mazuri hata kama matokeo hayo hayataendana na uwezo walio nao wanafunzi. Katika kutengeneza raslimali watu ya kutosha, Tanzania kama ilivyo kwa nchi nyingine haina namna ya kukwepa kuhakikisha kwamba mfumo wa elimu unaandaa vijana au wananchi wenye uwezo wa kukabiliana na changamoto zinazowakabili wao wenyewe, jamii na Taifa kwa ujumla; pia kuwa na wananchi ambao watakuwa na ujasiri, tija na ubunifu, katika uzalishaji katika shughuli na fursa mbalimbali watakazozipata au kuzitafuta. Hali hii haipatikani kwa kuhangaika na alama za ufaulu kama kipaumbele. Tunahitaji kuhangaika na mfumo wa utoaji elimu utakaotusaidia kuleta mapinduzi ya kweli ya kiuchumi, kijamii na kisiasa.
HakiElimu inaishauri Serikali kusitisha matumizi ya alama na madaraja haya mapya. Irudi kwa wadau na ushahidi kuhusu uamuzi huu; huku ikitoa nafasi ya kuchukua maoni ambayo yanaweza kuboresha mfumo wa upimaji wa wanafunzi. Wakati zoezi hilo linaendelea, HakiElimu inaisisitiza Serikali kutumia matokeo ya tafiti mbalimbali na mipango iliyopo kushughulikia dosari na changamoto zinazorudisha nyuma elimu yetu, hasa zile zinazokwamisha ufundishaji na ujifunzaji shuleni.
Tamko hili limesainiwa na,
Elizabeth Missokia Mkurugenzi Mtendaji, HakiElimu




